88 Unihuishe kwa fadhili zako,Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako.
89 Ee BWANA, neno lako lasimamaImara mbinguni hata milele.
90 Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi,Umeiweka nchi, nayo inakaa.
91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo,Maana vitu vyote ni watumishi wako.
92 Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu,Hapo ningalipotea katika taabu zangu.
93 Hata milele sitayasahau maagizo yako,Maana kwa hayo umenihuisha.
94 Mimi ni wako, uniokoe,Kwa maana nimejifunza mausia yako.