96 Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho,Bali agizo lako ni pana mno.
97 Sheria yako naipenda mno ajabu,Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.
98 Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu,Kwa maana ninayo sikuzote.
99 Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote,Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
100 Ninao ufahamu kuliko wazee,Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.
101 Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya,Ili nilitii neno lako.
102 Sikujiepusha na hukumu zako,Maana Wewe mwenyewe umenifundisha.