4 Sitaacha macho yangu kuwa na usingizi,Wala kope zangu kusinzia;
5 Hata nitakapompatia BWANA mahali,Na Shujaa wa Yakobo maskani.
6 Tazama, tulisikia habari zake katika Efrata,Katika konde la Yearimu tuliiona.
7 Na tuingie katika maskani yake,Tusujudu penye kiti cha kuwekea miguu yake.
8 Ee BWANA, uinuke, uende kwenye raha yako,Wewe na sanduku la nguvu zako.
9 Makuhani wako na wavikwe haki,Watauwa wako na washangilie.
10 Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako,Usiurudishe nyuma uso wa masihi wako.