8 Ee BWANA, uinuke, uende kwenye raha yako,Wewe na sanduku la nguvu zako.
9 Makuhani wako na wavikwe haki,Watauwa wako na washangilie.
10 Kwa ajili ya Daudi, mtumishi wako,Usiurudishe nyuma uso wa masihi wako.
11 BWANA amemwapia Daudi neno la kweli,Hatarudi nyuma akalihalifu,Baadhi ya wazao wa mwili wakoNitawaweka katika kiti chako cha enzi.
12 Wanao wakiyashika maagano yangu,Na shuhuda nitakazowafundisha;Watoto wao nao wataketiKatika kiti chako cha enzi milele.
13 Kwa kuwa BWANA ameichagua Sayuni,Ameitamani akae ndani yake.
14 Hapo ndipo mahali pangu pa raha milele,Hapo nitakaa kwa maana nimepatamani.