15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
16 Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
17 Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
18 Akawaua wafalme mashuhuri;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
19 Sihoni, mfalme wa Waamori;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
20 Na Ogu, mfalme wa Bashani;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
21 Akaitoa nchi yao iwe urithi;Kwa maana fadhili zake ni za milele.