3 Mshukuruni Bwana wa mabwana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
4 Yeye peke yake afanya maajabu makuu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
5 Yeye aliyefanya mbingu kwa fahamu zake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
6 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku;Kwa maana fadhili zake ni za milele.