6 Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
8 Jua litawale mchana;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
9 Mwezi na nyota zitawale usiku;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Akawatoa Waisraeli katikati yao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.