9 Mwezi na nyota zitawale usiku;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
10 Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wa kwanza wao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
11 Akawatoa Waisraeli katikati yao;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
13 Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
14 Akawavusha Israeli katikati yake;Kwa maana fadhili zake ni za milele.
15 Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;Kwa maana fadhili zake ni za milele.