1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote,Mbele ya miungu nitakuimbia zaburi.
2 Nitasujudu nikilikabili hekalu lako takatifu,Nitalishukuru jina lako,Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako,Kwa maana umeikuza ahadi yako,Kuliko jina lako lote.
3 Siku ile niliyokuita uliniitikia,Ukanifariji nafsi kwa kunitia nguvu.
4 Ee BWANA, wafalme wote wa dunia watakushukuru,Watakapoyasikia maneno ya kinywa chako.