1 Ee BWANA, umenichunguza na kunijua.
2 Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu;Umelifahamu wazo langu tokea mbali.
3 Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu,Umeelewa na njia zangu zote.
4 Maana hamna neno ulimini mwanguUsilolijua kabisa, BWANA.
5 Umenizingira nyuma na mbele,Ukaniwekea mkono wako.
6 Maarifa hayo ni ya ajabu, yanishinda mimi,Hayadirikiki, siwezi kuyafikia.
7 Niende wapi nijiepushe na roho yako?Niende wapi niukimbie uso wako?