11 Kama nikisema, Hakika giza litanifunika,Na nuru inizungukayo ingekuwa usiku;
12 Giza nalo halikufichi kitu,Bali usiku huangaza kama mchana;Giza na mwanga kwako ni sawasawa.
13 Maana Wewe ndiwe uliyeniumba mtima wangu,Uliniunga tumboni mwa mama yangu.
14 Nitakushukuru kwa kuwa nimeumbwaKwa jinsi ya ajabu ya kutisha.Matendo yako ni ya ajabu,Na nafsi yangu yajua sana,
15 Mifupa yangu haikusitirika kwako,Nilipoumbwa kwa siri,Nilipoungwa kwa ustadi pande za chini za nchi;
16 Macho yako yaliniona kabla sijakamilika;Chuoni mwako ziliandikwa zote pia,Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.
17 Mungu, fikira zako zina thamani nyingi kwangu;Jinsi ilivyo kubwa jumla yake!