5 Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili;Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani;Kichwa changu kisikatae,Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.
6 Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge,Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.
7 Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi,Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.
8 Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana,Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu.
9 Unilinde na mtego walionitegea,Na matanzi yao watendao maovu.