4 Kizazi kwa kizazi kitayasifu matendo yako,Kitayatangaza matendo yako makuu.
5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako,Na matendo yako yote ya ajabu.
6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha,Nami nitausimulia ukuu wako.
7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu.Wataiimba haki yako.
8 BWANA ana fadhili, ni mwingi wa huruma,Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9 BWANA ni mwema kwa watu wote,Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.
10 Ee BWANA, kazi zako zote zitakushukuru,Na wacha Mungu wako watakuhimidi.