5 Nitaifikiri fahari ya utukufu wa adhama yako,Na matendo yako yote ya ajabu.
6 Watu watayataja matendo yako ya kutisha,Nami nitausimulia ukuu wako.
7 Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu.Wataiimba haki yako.
8 BWANA ana fadhili, ni mwingi wa huruma,Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema,
9 BWANA ni mwema kwa watu wote,Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.
10 Ee BWANA, kazi zako zote zitakushukuru,Na wacha Mungu wako watakuhimidi.
11 Wataunena utukufu wa ufalme wako,Na kuuhadithia uweza wako.