9 Milima na vilima vyote,Miti yenye matunda na mierezi yote.
10 Hayawani, na wanyama wafugwao,Vitambaavyo, na ndege wenye mbawa.
11 Wafalme wa dunia, na watu wote,Wakuu, na makadhi wote wa dunia.
12 Vijana waume, na wanawali,Wazee, na watoto;
13 Na walisifu jina la BWANA,Maana jina lake peke yake limetukuka;Adhama yake i juu ya nchi na mbingu.