21 Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.
22 Hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu,Wala amri zake sikujiepusha nazo.
23 Nami nalikuwa mkamilifu mbele zake,Nikajilinda na uovu wangu.
24 Mradi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu,Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
25 Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili;Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
26 Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu;Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.
27 Maana Wewe utawaokoa watu wanaoonewa,Na macho ya kiburi utayadhili.