38 Nitawapiga-piga wasiweze kusimama,Wataanguka chini ya miguu yangu.
39 Nawe hunifunga mshipi wa nguvu kwa vita,Hunitiishia chini yangu walioniondokea.
40 Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Nao walionichukia nimewakatilia mbali.
41 Walipiga yowe, lakini hakuna wa kuokoa,Walimwita BWANA lakini hakuwajibu,
42 Nikawaponda kama mavumbi mbele ya upepo,Nikawatupa nje kama matope ya njiani.
43 Umeniokoa na mashindano ya watu,Umenifanya niwe kichwa cha mataifa.Watu nisiowajua walinitumikia.
44 Kwa kusikia tu habari zangu,Mara wakanitii.Wageni walinijia wakinyenyekea.