1 BWANA akujibu siku ya dhiki,Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.
2 Akupelekee msaada toka patakatifu pake,Na kukutegemeza toka Sayuni.
3 Azikumbuke sadaka zako zote,Na kuzitakabali dhabihu zako.
4 Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako,Na kuyatimiza mashauri yako yote.