9 Naam, Wewe ndiwe uliyenitoa tumboni,Ulinitumainisha matitini mwa mama yangu.
10 Kwako nalitupwa tangu tumboni,Toka tumboni mwa mamangu ndiwe Mungu wangu.
11 Usiwe mbali nami maana taabu i karibu,Kwa maana hakuna msaidizi.
12 Mafahali wengi wamenizunguka,Walio hodari wa Bashani wamenisonga;
13 Wananifumbulia vinywa vyao,Kama simba apapuraye na kunguruma.
14 Nimemwagika kama maji,Mifupa yangu yote imeteguka,Moyo wangu umekuwa kama nta,Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.
15 Nguvu zangu zimekauka kama gae,Ulimi wangu waambatana na taya zangu;Unaniweka katika mavumbi ya mauti