3 Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja;Wataaibika watendao uhaini bila sababu.
4 Ee BWANA, unijulishe njia zako,Unifundishe mapito yako,
5 Uniongoze katika kweli yako,Na kunifundisha.Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu,Nakungoja Wewe mchana kutwa.
6 Ee BWANA, kumbuka rehema zako na fadhili zako,Maana zimekuwako tokea zamani.
7 Usiyakumbuke makosa ya ujana wangu,Wala maasi yangu.Unikumbuke kwa kadiri ya fadhili zako,Ee BWANA kwa ajili ya wema wako.
8 BWANA yu mwema, mwenye adili,Kwa hiyo atawafundisha wenye dhambi njia.
9 Wenye upole atawaongoza katika hukumu,Wenye upole atawafundisha njia yake.