1 Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.
2 Ee BWANA, Mungu wangu,Nalikulilia ukaniponya.
3 Umeniinua nafsi yangu,Ee BWANA, kutoka kuzimu.Umenihuisha na kunitoaMiongoni mwao washukao shimoni.
4 Mwimbieni BWANA zaburi,Enyi watauwa wake.Na kufanya shukrani.Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.