16 Umwangaze mtumishi wakoKwa nuru ya uso wako;Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
17 Ee BWANA, nisiaibishwe, maana nimekuita;Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni.
18 Midomo ya uongo iwe na ububu,Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi,Kwa majivuno na dharau.
19 Jinsi zilivyo nyingi fadhili zakoUlizowawekea wakuchao;Ulizowatendea wakukimbiliaoMbele ya wanadamu!
20 Utawasitiri na fitina za watuKatika sitara ya kuwapo kwako;Utawaficha katika hemaNa mashindano ya ndimi.
21 BWANA ahimidiwe; kwa maana amenitendeaFadhili za ajabu katika mji wenye boma.
22 Nami nalisema kwa haraka yangu,Nimekatiliwa mbali na macho yako;Lakini ulisikia sauti ya dua yanguWakati nilipokulilia.