19 Walio adui zangu bure wasinisimange,Wanaonichukia bila sababu wasining’ong’e.
20 Maana hawasemi maneno ya amani,Na juu ya watulivu wa nchi huwaza hila.
21 Nao wananifumbulia vinywa vyao,Husema, Ewe! Ewe! Jicho letu limeona.
22 Wewe, BWANA, umeona, usinyamaze;Ee Bwana, usiwe mbali nami.
23 Uamke, uwe macho ili kunipatia hukumuKwa ajili ya madai yangu,Mungu wangu na Bwana wangu.
24 Unihukumu kwa haki yako,Ee BWANA, Mungu wangu,Wala wasinisimangize.
25 Wasiseme moyoni, Haya! Ndivyo tutakavyo;Wasiseme, Tumemmeza.