1 Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya,Usiwahusudu wafanyao ubatili.
2 Maana kama majani watakatika mara,Kama miche mibichi watanyauka.
3 Umtumaini BWANA ukatende mema,Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu.
4 Nawe utajifurahisha kwa BWANA,Naye atakupa haja za moyo wako.
5 Umkabidhi BWANA njia yako,Pia umtumaini, naye atafanya.