36 Nikapita na kumbe! Hayuko,Nikamtafuta wala hakuonekana.
37 Umwangalie sana mtu mkamilifu,Umtazame mtu mnyofu,Maana mwisho wake mtu huyo ni amani.
38 Wakosaji wataangamizwa pamoja,Wasio haki mwisho wao wataharibiwa.
39 Na wokovu wa wenye haki una BWANA;Yeye ni ngome yao wakati wa taabu.