3 Hamna uzima katika mwili wanguKwa sababu ya ghadhabu yako.Wala hamna amani mifupani mwanguKwa sababu ya hatia zangu.
4 Maana dhambi zangu zimenifunikiza kichwa,Kama mzigo mzito zimenilemea mno.
5 Jeraha zangu zinanuka, zimeoza,Kwa sababu ya upumbavu wangu.
6 Nimepindika na kuinama sana,Mchana kutwa nimekwenda nikihuzunika.
7 Maana viuno vyangu vimejaa homa,Wala hamna uzima katika mwili wangu.
8 Nimedhoofika na kuchubuka sana,Nimeugua kwa fadhaa ya moyo wangu.
9 Bwana, haja zangu zote ziko mbele zako,Kuugua kwangu hakukusitirika kwako.