3 BWANA atamtegemeza alipo mgonjwa kitandani.Katika ugonjwa wake umemtandikia.
4 Nami nalisema, BWANA, unifadhili,Uniponye roho yangu maana nimekutenda dhambi.
5 Adui zangu wananitaja kwa maneno mabaya,Atakufa lini, jina lake likapotea?
6 Na mmoja wao akija kunitazama asema uongo,Moyo wake hujikusanyia maovu,Naye atokapo nje huyanena.
7 Wote wanaonichukia wananinong’ona,Wananiwazia mabaya.
8 Neno la kisirani limemgandama,Na iwapo amelala hatasimama tena.
9 Msiri wangu tena niliyemtumaini,Aliyekula chakula changu,Ameniinulia kisigino chake.