16 Kwa sauti ya mwenye kulaumu na kukufuru,Kwa sababu ya adui na mjilipiza kisasi.
17 Haya yote yametupata, bali hatukukusahau,Wala hatukulihalifu agano lako.
18 Hatukuiacha mioyo yetu irudi nyuma,Wala hatua zetu hazikuiacha njia yako.
19 Hata utuponde katika kao la mbwa-mwitu,Na kutufunika kwa uvuli wa mauti.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu,Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu;
21 Je! Mungu hatalichunguza neno hilo?Maana ndiye azijuaye siri za moyo.
22 Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa.