1 Moyo wangu umefurika kwa neno jema,Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme;Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.
2 Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu;Neema imemiminiwa midomoni mwako,Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.
3 Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari,Utukufu ni wako na fahari ni yako.
4 Katika fahari yako usitawi uendeleeKwa ajili ya kweli na upole na hakiNa mkono wako wa kuumeUtakufundisha mambo ya kutisha.
5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako;Imo mioyoni mwa adui za mfalme.