5 Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako;Imo mioyoni mwa adui za mfalme.
6 Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele,Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
7 Umeipenda haki;Umeichukia dhuluma.Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta,Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8 Mavazi yako yote hunukia manemaneNa udi na mdalasini.Katika majumba ya pembeVinubi vimekufurahisha.
9 Binti za wafalme wamoMiongoni mwa akina bibi wako wastahiki.Mkono wako wa kuume amesimama malkiaAmevaa dhahabu ya Ofiri.
10 Sikia, binti, utazame, utege sikio lako,Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11 Naye mfalme atautamani uzuri wako,Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.