19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya,Na ulimi wako watunga hila.
20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako,Na mwana wa mama yako umemsingizia.
21 Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza;Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe.Walakini nitakukemea;Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.
22 Yafahamuni hayo,Ninyi mnaomsahau Mungu,Nisije nikawararueni,Asipatikane mwenye kuwaponya.