6 Na mbingu zitatangaza haki yake,Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.
7 Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena,Mimi nitakushuhudia, Israeli;Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.
8 Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako,Na kafara zako ziko mbele zangu daima.
9 Sitatwaa ng’ombe katika nyumba yako,Wala beberu katika mazizi yako.
10 Maana kila hayawani ni wangu,Na makundi juu ya milima elfu.
11 Nawajua ndege wote wa milima,Na wanyama wote wa mashamba ni wangu
12 Kama ningekuwa na njaa singekuambia,Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.