1 Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari?Wema wa Mungu upo sikuzote.
2 Ulimi wako watunga madhara,Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila
3 Umependa mabaya kuliko mema,Na uongo kuliko kusema kweli.
4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu,Ewe ulimi wenye hila.
5 Lakini Mungu atakuharibu hata milele;Atakuondolea mbali;Atakunyakua hemani mwako;Atakung’oa katika nchi ya walio hai.