1 Ee Mungu, ukisikie kilio changu,Uyasikilize maombi yangu.
2 Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo,Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.
3 Kwa maana ulikuwa kimbilio langu,Ngome yenye nguvu adui asinipate.
4 Nitakaa katika hema yako milele,Nitaikimbilia sitara ya mbawa zako