1 Nafsi yangu yamngoja Mungu peke yake kwa kimya,Wokovu wangu hutoka kwake.
2 Yeye tu ndiye mwamba wangu na wokovu wangu,Ngome yangu, sitatikisika sana.
3 Hata lini mtamshambulia mtu,Mpate kumwua ninyi nyote pamoja?Kama ukuta unaoinama,Kama kitalu kilicho tayari kuanguka,
4 Hufanya shauri kumwangusha tu katika cheo chake;Huufurahia uongo.Kwa kinywa chao hubariki;Kwa moyo wao hulaani.
5 Nafsi yangu, umngoje Mungu peke yake kwa kimya.Tumaini langu hutoka kwake.