7 Maana Wewe umekuwa msaada wangu,Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.
8 Nafsi yangu inakuandama sana;Mkono wako wa kuume unanitegemeza.
9 Bali waitafutao nafsi yangu, ili kuiharibu,Wataingia pande za nchi zilizo chini.
10 Watatolewa wafe kwa nguvu za upanga,Watakuwa riziki za mbwa-mwitu.