1 Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,Na mwana wa mfalme haki yako.
2 Atawaamua watu wako kwa haki,Na watu wako walioonewa kwa hukumu.
3 Milima itawazalia watu amani,Na vilima navyo kwa haki.
4 Atawahukumu walioonewa wa watu,Atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea.