4 Atawahukumu walioonewa wa watu,Atawaokoa wahitaji, atamseta mwenye kuonea.
5 Watakuogopa wakati wote wa kudumu jua,Na wakati wa kung’aa mwezi kizazi hata kizazi.
6 Atashuka kama mvua juu ya majani yaliyokatwa,Kama manyunyu yainyweshayo nchi.
7 Siku zake yeye, mtu mwenye haki atasitawi,Na wingi wa amani hata mwezi utakapokoma.
8 Na awe na enzi toka bahari hata bahari,Toka Mto hata miisho ya dunia.
9 Wakaao jangwani na wainame mbele zake;Adui zake na warambe mavumbi.
10 Wafalme wa Tarshishi na visiwa na walete kodi;Wafalme wa Sheba na Seba na watoe vipawa.