18 Hakika Wewe huwaweka penye utelezi,Huwaangusha mpaka palipoharibika.
19 Namna gani wamekuwa ukiwa mara!Wametokomea na kutoweshwa kwa utisho.
20 Ee Bwana, kama ndoto wakati wa kuamka,Uondokapo utaidharau sanamu yao.
21 Moyo wangu ulipoona uchungu,Viuno vyangu viliponichoma,
22 Nalikuwa kama mjinga, sijui neno;Nalikuwa kama mnyama tu mbele zako.
23 Walakini mimi ni pamoja nawe daima,Umenishika mkono wa kuume.
24 Utaniongoza kwa shauri lako,Na baadaye utanikaribisha kwa utukufu.