6 Na sasa nakishi yake yote piaWanaivunja-vunja kwa mashoka na nyundo.
7 Wamepatia moto patakatifu pako;Wamelinajisi kao la jina lako hata chini.
8 Walisema mioyoni mwao,Na tuwaangamize kabisa;Mahali penye mikutano ya MunguWamepachoma moto katika nchi pia.
9 Hatuzioni ishara zetu, wala sasa hakuna nabii,Wala kwetu hakuna ajuaye, hata lini?
10 Ee Mungu, mtesi atalaumu hata lini?Adui alidharau jina lako hata milele?
11 Mbona unaurudisha mkono wako,Naam, mkono wako wa kuume,Uutoe kifuani mwako,Ukawaangamize kabisa.
12 Lakini Mungu ni mfalme wangu tokea zamani,Afanyaye mambo ya wokovu katikati ya nchi.