1 Nimpazie Mungu sauti yangu,Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.
2 Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana;Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea;Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3 Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika;Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
4 Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike;Naliona mashaka nisiweze kunena.