11 Nitayakumbuka matendo ya BWANA;Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.
12 Pia nitaitafakari kazi yako yote;Nitaziwaza habari za matendo yako.
13 Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu;Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?
14 Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu;Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.
15 Kwa mkono wako umewakomboa watu wako,Wana wa Yakobo na Yusufu.
16 Ee Mungu, yale maji yalikuona,Yale maji yalikuona, yakaogopa.Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
17 Mawingu yakamwaga maji.Mbingu nazo zikatoa sauti,Mishale yako nayo ikatapakaa.