15 Kwa mkono wako umewakomboa watu wako,Wana wa Yakobo na Yusufu.
16 Ee Mungu, yale maji yalikuona,Yale maji yalikuona, yakaogopa.Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
17 Mawingu yakamwaga maji.Mbingu nazo zikatoa sauti,Mishale yako nayo ikatapakaa.
18 Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli;Umeme uliuangaza ulimwengu.Nchi ilitetemeka na kutikisika;
19 Njia yako ilikuwa katika bahari.Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu;Hatua zako hazikujulikana.