16 Ee Mungu, yale maji yalikuona,Yale maji yalikuona, yakaogopa.Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
17 Mawingu yakamwaga maji.Mbingu nazo zikatoa sauti,Mishale yako nayo ikatapakaa.
18 Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli;Umeme uliuangaza ulimwengu.Nchi ilitetemeka na kutikisika;
19 Njia yako ilikuwa katika bahari.Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu;Hatua zako hazikujulikana.