2 Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana;Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea;Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3 Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika;Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
4 Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike;Naliona mashaka nisiweze kunena.
5 Nalifikiri habari za siku za kale,Miaka ya zamani zilizopita.
6 Nakumbuka wimbo wangu usiku,Nawaza moyoni mwangu,Roho yangu ikatafuta.
7 Je! Bwana atatupa milele na milele?Hatatenda fadhili tena kabisa?
8 Rehema zake zimekoma hata milele?Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?