11 Wakayasahau matendo yake,Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.
12 Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu,Katika nchi ya Misri, konde la Soani.
13 Aliipasua bahari akawavusha;Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.
14 Akawaongoza kwa wingu mchana,Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
15 Akapasua miamba jangwani;Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
16 Akatokeza na vijito gengeni,Akatelemsha maji kama mito.
17 Lakini wakazidi kumtenda dhambi,Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.