56 Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi,Wala hawakuzishika shuhuda zake.
57 Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao;Wakaepea kama upinde usiofaa.
58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
59 Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.
60 Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
61 Akaziacha nguvu zake kutekwa,Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
62 Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga;Akaughadhibikia urithi wake.