58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu,Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
59 Mungu akasikia, akaghadhibika,Akamkataa Israeli kabisa.
60 Akaiacha maskani ya Shilo,Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
61 Akaziacha nguvu zake kutekwa,Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
62 Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga;Akaughadhibikia urithi wake.
63 Moto ukawala vijana wao,Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
64 Makuhani wao walianguka kwa upanga,Wala wajane wao hawakuomboleza.