5 Ee BWANA, hata lini? Utaona hasira milele?Wivu wako utawaka kama moto?
6 Ukali wako uwamwagie mataifa wasiokujua,Na falme za hao wasioliitia jina lako.
7 Kwa maana wamemla Yakobo,Na matuo yake wameyaharibu.
8 Usikumbuke juu yetu maovu ya baba zetu,Rehema zako zije kutulaki hima,Kwa maana tumedhilika sana.
9 Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie,Kwa ajili ya utukufu wa jina lako.Utuokoe, utughofiri dhambi zetu,Kwa ajili ya jina lako.
10 Kwa nini mataifa kusema,Yuko wapi Mungu wao?Kisasi cha damu ya watumishi wako iliyomwagikaKijulike kati ya mataifa machoni petu.
11 Kuugua kwake aliyefungwaNa kuingie mbele zako.Kwa kadiri ya uweza wa mkono wakoUwahifadhi wana wa mauti.