8 Na nisikie atakavyosema Mungu BWANA,Maana atawaambia watu wake amani,Naam, na watauwa wake pia,Bali wasiurudie upumbavu tena.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wamchao,Utukufu ukae katika nchi yetu.
10 Fadhili na kweli zimekutana,Haki na amani zimehusiana.
11 Kweli imechipuka katika nchi,Haki imechungulia kutoka mbinguni.
12 Naam, BWANA atatoa kilicho chema,Na nchi yetu itatoa mazao yake.